![]() |
Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Mali Cheick Modibo Diarra |
Waziri Mkuu wa Mali Cheick Modibo Diarra amejiuzulu wadhifa wake saa
chache baada ya kukamatwa na wanajeshi waliomkuta nyumbani kwake.
Kujiuzulu huko kunaupeleka pabaya zaidi mzozo unaoendelea kuikumba nchi
hiyo.
Tangazo la Cheick Modibo Diarra kujiuzulu wadhifa wake ambalo limerushwa
na kituo cha taifa cha utangazaji, lilikuwa fupi. ''Mimi Cheick Modibo
Diarra najiuzulu pamoja na serikali yangu'', alisema katika tangazo hilo
katika sauti yenye unyonge. Aliwashukuru wanamuunga mkono na kuelezea
matumaini kwamba atakayechukua nafasi yake atakuwa na mafanikio.Ujumbe wake huo ulitolewa saa kadhaa baada ya taarifa kutoka kwa watu walio karibu naye, kwamba waziri mkuu alikuwa amekamatwa na wanajeshi 20 kutoka kambi ya Kati iliyoko nje kidogo ya mji mkuu, Bamako, ambayo ni makao makuu ya wanajeshi walioiangusha serikali mwezi Machi mwaka huu. Taarifa hizo zilidai kuwa wanajeshi hao walipewa amri na aliyekuwa kiongozi wa mapinduzi hayo, Kapteni Amadou Sanogo. Afisa mmoja wa usalama alithibitisha taarifa hiyo baadaye.
Mkono wa Kapteni Sanogo
![]() |
Kapteni Amadou Haya Sanogo, kiongozi wa mapinduzi ya |
Cheick Modibo Diarra aliteuliwa kuwa waziri mkuu wiki chache baada ya mapinduzi ya mwezi Machi ambayo yaliitumbukiza Mali, ambayo hapo awali ilikuwa na utawala imara wa kidemokrasia, katika mzozo ambao umesababisha sehemu yake kubwa ya kaskazini kuangukia mikononi mwa wanamgambo wenye itikadi kali ya kiislamu.
Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 60 anaunga mkono kuletwa kwa wanajeshi kutoka nchi za kanda ya Afrika magharibi, kusaidia kuwafukuza wanamgambo hao wanaoishikilia sehemu ya kaskazini. Kapteni Sanogo anaupinga vikali mpango huo.
Tofauti juu ya kuletwa vikosi vya nje

Hata hivyo, makundi hayo sasa yamefarakana, na wanamgambo wa kiislamu ndio wanaoishikilia sehemu ya kaskazini baada ya kuwatimua watuareg. Nchi za Afrika Magharibi zinaliwekea shinikizo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuupitisha mpango wa kuingilia kijeshi kuikomboa kaskazini ya Mali, mpango ambao unaungwa mkono na Ufaransa.
Nchi za magharibi zinahofia kuwa sehemu hiyo inaweza kugeuka maficho ya makundi ya kigaidi. Umoja wa Ulaya jana uliafiki mpango wa kupelekwa kwa maafisa watakaotoa mafunzo kuisaidia Mali kulirejesha eneo lake la kaskazini kutoka mikononi mwa wanamgambo hao. Marekani na Umoja wa Mataifa wanataka tahadhari zaidi ichukuliwe kukabiliana na wanamgambo hao.
Mwandishi: Daniel Gakuba/AFPE
Mhariri:Josephat Charo
Chanzo na -DW
No comments:
Post a Comment