Awilo Longomba alizaliwa huko Kinshasa, zamani ikifahamika
kama Léopoldville. Baba yake alitokea katika mkoa wa Mongo-Ecuador, Mama yake
pia ni mwenyeji wa huko katika Mkoa wa Ngombe ya Congo Brazzaville.
Awilo Longomba ni mwanamuziki wa Kongo ambaye alikuwa mpiga ngoma katika
bendi za Viva la Musica, Stukas, Nouvelle Generation na Loketo.
Mwaka wa 1995, hatimaye aliacha kupiga
ngoma na kuamua kuimba ambapo alitoa albamu yake ya kwanza, aliyoiita Moto Pamba, baada ya kupata msaada kutoka kwa watu kama akina Shimita, Ballou Canta, Dindo Yogo, Dally Kimoko,Sam Mangwana, Syran Mbenza na Rigo Star.
Album yake ya pili, Coupe Bibamba aliitoa mwaka wa 1998ambayo ilimfanya ajulikane kote barani Afrika, Ulaya
na Amerika.
Hii ilifuatiwa na Kafou Kafou ya mwaka wa 2001 na albamu yake ya
hivi karibuni, Mondongo iliyotoka mwaka wa 2004, ambayo
inawashirikisha akina Japponais, Dally Kimoko, Caen Madoka, Djudjuchet, Josky na Simaro Lutumba.
Pia alishirikishwa kama atalaku (mtu wa
kutumbuiza) katika baadhi ya rekodi za soukous.
Awilo kwa sasa anaishi nchini Ufaransa .
AWlo amezaliwa katika Familia ya
MUZIKI:- Ikiwa ni pamoja na baba yake Victor Longomba mwanachama
mwanzilishi wa TP OK Jazz na vilevile Longombas ambalo ni kundi
maarufu la afro-fusion lenye makao nchini Kenya.
Mnamo mwaka wa 2008 Awilo Longomba alitoa albamu mpya, ya SUPER-MAN,
ambayo ilikuwa fanikio kubwa.
Awilo amefanikiwa kupata umaarufu si Afrika tu, bali hata Marekani / Kanada huku akiwa katika ziara
pamoja na Nabtry International Cultural Dancers (kundi la kitamaduni la
kimataifa la kusakata au kucheza ngoma) kundi la Kiafrika la kucheza ngoma lililoanzishwa
mwaka wa 2007 na Grace Haukwa.
Awilo,kupitia Album yake ya Super Man
amefanikiwa kupata TUZO LA MTUMBUIZAJI
BORA WA SOUKOUS WA MWAKA WA 2009.
Penye nia,pana njia. Ni kwa jitihada kama alivyo fanya,amini inawezekana kufanikiwa.
No comments:
Post a Comment