Unaambiwa Mwanaume kazi!Hii ni Ngara
Na Shaaban ndyamukama-ngarakwetublogspot.com
Mchimbaji Elias Zacharia akitoka shimon |
Mchimbaji anayefahamika kwajina la Nzigiyimana akiwa nje ya Shimo la futi 60 |
Vijana wawili wanaokadiriwa kuwa na umri wa miaka 35 na 40
wanaishi katika mazingira hatarishi katika pori la Nyanzari na Nyakafandi
wilaya ya Ngara mkoani Kagera wakitafuta
maisha kwa kuchimba na kupasua miamba kwa mkono
ili kuweza kupata madini ya dhahabu wakitumia mikono kuchimba kupasua
miamba
Wakiongea na mwandishi wa habari hizi katika pori la maeneo hayo
vijana hao wamesema wanatafuta madini aina ya Dhahabu na uchimbaji wake ni
mugumu kutokana na shimo kuwa na mwamba unaosababisha kushindwa kufikia dhahabu
umbali wa futi 70 kupata madini hayo
Mmoja wa vijana hao Nizigimana Samsoni mkazi wa wilayani
Geita amesema kuwa wako katika kata zaRulenge na Muganza wilayani Ngara wakichimba na kupasua miamba kutafuta dhahabu ambapo shimo wanalolichimba
limefikia urefu wa futi 60 tangu mwezi februari mwaka huu hadi sasa
Samsoni alisema katika kujitafutia ajira wanachimba na
kupasua mawe kwenye miamba na tayari wamepata madini ya Nickel na mawe aina ya
Qwagis na wataalamu wao wa madini walioko mkoani Geita wamefanya uchunguzi na
kubaini kuwa dhahabu inaweza kupatikana kati ya futi 66 hadi 70.
Alisema mawe meupe yanayofanana na glasi wameagiza wateja wa
kununua mawe hayo kwani wapimapo mchanga kwa vipimo vya asili kwa kutumia karai na maji wameshagundua
cheche za kuwepo dhahabu na kuleta matumaini ya kupata madini hayo.Aliongeza
kuwa katika kujitafutia ajira ya
kuchimba shimo hilo na kupasua mwamba tangu waanze mwezi februari mwaka huu viongozi wa kijiji cha Rulenge na Mukubu nawale
wa kata ya Muganza kata wamekuwa
wakiwakamata vijana hao kwa madai ya kuharibu mazingira na kuwakatisha tamaa
vijana wengine wanaohitaji kujiajiri kwa kutumia nguvu zao
Alidai kuwa wanatumia nyenzo duni za kufanyia kazi na shughuli yao kuwa ngumu
kwani wanatumia magunia ya kubebea mawe na udongo wakifunga kamba kuvuta udongo
au vipande vya mawe kutoka shimoni na
kuchelewa kutimiza malengo yao
ya kupata dhahabu mapema .“Zana tunazotumia
kutafuta madini ya dhahabu ni nyundo na tindo kupasua mawe katika miamba
na huvuta kamba iliyofunga gunia la udongo au vipande vya mawe toka shimoni kwa
kuzungusha gogo lililo katika miti miwili ya matawi kama
mashine kurahisisha uvutaji wa mzigo kwa urahisi”.Alisema
Kwa upande wake
Elias Zacharia amesema kuwa changamoto nyingine ni ukosefu wa kituo cha kupata
matibabu mara wapatapo msukosuko wa kiafya na hulazimika kutembea umbali mrefu
kwenda kutafuta matibabu Mukubu ,Munjebwe au Bukiriro ambapo ni mbali na makazi
yao
Alisema kuwa mara washindwapo kufika kwenye vituo vya huduma
za afya hulazimika kuwatafuta watu wa kwenda kuwanunulia dawa katika maduka ya
dawa baridi katika mji mdogo wa Rulenge
ili kuzuia kwa muda vinyemelezi vya magonjwa pasipo kupima au kupata ushauri wa
maafisa tiba za binadamu
Hata hivyo viongozi wa vitongoji vijiji na kata walipohojiwa
kuhusu vijana hao walidai madini yanayopatikana eneo hilo ni aina ya Nickel ambapo makampuni
kadhaa yamefika na kupima na upatikanaji wake ni kutumia mashine sio mikono.
Afisa mtendaji wa kata ya Rulenge Richard Sentoz na Diwani wa hiyo Hamis Baliyanga walisema
kuwa vijana hao wakishindwa kupata wanachotafuta watarudi katika familia
zao kuendelea na shughuli za maisha yao
kama kawaida ili mradi walinde mazingira wanayotumia.
Eneo la Nyakafandi ,Nyanzari na maeneo mengine katika kata
za Rulenge Muganza Bugarama pamoja
Bukiriro yanafanyiwa utafiti mara kwa mara na kampuni ya Kabanga Nickel tangu
mwaka 2005 kuwa na madini ya dhahabu ,Nickel ,a madini mengineyo ambapo serikali
inatarajia kufungua mgodi wa Nickel utakao dumu miaka 25 hadi 30 (under ground
)na mchakato wa kuhamisha walio ndani ya mradi umeanza ili wahusika waweze
kulipwa fidia ya mali walizo nazo katika eneo la mradi.
Habari imeandikwa
na Shaaban Ndyamukama
No comments:
Post a Comment