February 11, 2016

MAGODORO YANAYOTOKANA NA MIFUKO YA PLASTTIKI

Mwananchi aliyeajiriwa na Mohamed Semdoe, akisafisha Mifuko baada ya kuikusanya

majaribio ya Godoro

Mohamed Semdoe,mgunduzi na mtengenezaji wa Godoro

Mifuko ikiwa katika hatua za awali kutengeneza Godoro


Godoro likiwa tayari kwaajili ya Matumizi


MAGODORO YANAYOTOKANA NA MIFUKO YA PLASTIKI

WAZO LILILOANZISHWA NA KUBUNIWA NA MKUU WA IDARA YA MAZINGIRA KATIKA WILAYA YA KIBONDO MKOANI KIGOMA BW.MOHAMED SEMDOE
MHITIMU WA CHUO KIKUU CHA MZUMBE 2014/15
KIBONDO DISTRICT COUNCIL

ANAPATIKANA KWA SIMU NO. 0767830269/0784830269
AU BARUA PEPE  mohamedsemdoe@gmail.com
COPYRIGHT@TZ/T/2015/001677 GREEN MATTRESS of MOHAMED SEMDOE


Katika mazungumzo yake na mimi ameniambia kuwa wazo lake linatokana na kuhakikisha kuwa jamii inapunguza tatizo la kuzagaa kwa mifuko hiyo,na badala ya kuiacha ikichafua mazingira ikusanywe na kutengenezea bidhaa inayoinufaisha jamii usika.

Aidha, Bw. Semdoe anasema matazamio yake ni kuona Miji na vijiji inaepukana na kuzagaa kwa mifuko hiyo ifikapo 2020, na kama Fedha zikipatikana kwaajili ya kuendeshea mradi huo anategemea kupanua wigo wa shughuli kutoka katika wilaya ya Kibondo kwa sasa na kufikia maeneo 20 hadi majiji 5,Manispaa 5,Halmashauri 5,na Halmashauri za miji 5 ndani ya kipindi cha miaka miwili.
Hata hivyo,hadi kufikia sasa amefanikiwa kutengeneza magodoro 6 ambayo ameyagawa kwa jamii kulingana na mahitaji ya wahusika.

No comments:

Post a Comment