August 1, 2012

UFAFANUZI KUHUS FAO LA KUJITOA KATIKA MAREKEBISHO YA SHERIA ZA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII.

Kumb. Na. AE/164/334/Vol.II/2

Makamu wa Rais, Corporate Affairs
Barrick Gold
S.L.P 1081
Dar-es-Salaam

UFAFANUZI KUHUS FAO LA KUJITOA KATIKA MAREKEBISHO YA SHERIA ZA
MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII.

Ufuatao ni ufafanuzi mfupi kuhusu marekebisho ya Sheria za Mifuko hasa kuhusu fao
la kujitoa.

20 JULAI, 2012

1. Kama mtakumbuka Sheria za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na Sheria ya
Mamlaka zimefanyiwa marekebisho na kupitishwa na Bunge tarehe 13 Aprili,
2012. Sheria hiyo tayari imeshasaininiwa na Mheshimiwa Rais na imeanza
kutumika rasmi. Marekebisho haya yanawahusu wafanyakazi wote nchini
mwetu bila kubagua sekta yoyote ile.

2. Kwa mujibu wa marekebisho hayo fao la kujitoa (withdrawal benefits)
yamefutwa na kuanzia sasa hayatakuwepo. Mafao hayo yalikuwa yanatolewa
pale mwanachama alipokuwa anaacha kazi. Sasa mwanachama wa Mfuko
atapata mafao yake pale atakopfikisha umri wa kustaafu kwa hiari (miaka 55)
au kwa lazima (miaka 60) au pale anapopata ulemavu wa kudumu.

3. Kwa kuzuia fao la kujitoa mwanachama anapata fursa ya kupata mikopo ya
nyumba kwa kutumia dhamana ya michango yake kama ilivyoelezwa kwenye
Sheria ya SSRA kipengele cha 38.

4. Marekebisho hayo kuhusu kuzuia mafao ya kujitoa yamefanyika ili kutimiza
lengo na madhumuni ya hifadhi ya jamii ambayo ni kuhakikisha kuwa
mwanachama anapostaafu anapata mafao bora yatakayomwezesha kumudu
maisha ya uzeeni wakati ambapo nguvu ya kufanya kazi tayari imeshamwishia.
Mafao ya kujitoa yanapunguza na hata kuondoa kabisa kinga ya mfanyakazi
pale anapoumia kazini au anapofika uzeeni.

5. Tunawaomba muwaelimishe wafanyakazi umuhimu na madhumuni ya mafao ya
hifadhi ya jamii. Hifadhi ya jamii ni nyenzo mahususi iliyowekwa kuwasaidia
1

wafanyakazi kuendesha maisha yao wakati wanapokuwa wameishastaafu
tayari. Umasikini wa kipato wakati wa uzee ni mojawapo ya changamoto ngumu
kukabiliana nazo kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla. Tunawasihi tena
muelimishe wafanyakazi kuhusu jambo hili. Tafadhali msisite kuwasiliana na
Mamlaka pale ufafanuzi zaidi utakapohitajika

6. Kwa kuwa marekebisho hayo yamesainiwa na kuanza kutumika rasmi kama
sheria, mafao ya kujitoa hayawezi kutolewa tena na wafanyakazi watakaoacha
kazi kwa sababu ya marekebisho ya kipengele hicho watakuwa hawajaijitendea
haki wao wenyewe na pia itakuwa ni kunyume cha Sheria. Mamlaka inaandaa
kanuni za mafao ambayo lengo lake ni kuboresha maslahi ya wanachama,
kanuni hizo zitajadiliwa na wadau wakiwemo vyama vya wafanyakazi na waajiri
ili kupata maoni yao.

7. Tafadhali muwaelimishe wafanyakazi kwamba pamoja na kuzuia fao la kujitoa,
mafao mengine ambayo ni muhimu kwa sekta ya Madini yataendelea kutolewa
kama kawaida. Mafao hayo ni Kama vile kuumia kazini pamoja na fao la
ulemavu

8. Tumesikia kwamba tayari kuna hofu imejijenga kwa wanachama kuhusiana na
fao la kujitoa. Ikumbukwe kwamba baadhi ya Mifuko ilikuwa inatoa fao hilo
kinyume cha Sheria kwani katika Sheria zao hakuna fao la kujitoa. Tunapenda
kusisitiza kwamba wanachama wawe watulivu wakisubiri miongozo.

9. Tunapenda kuwahakikishia kwamba katika hili maslahi ya wanachama
yatalindwa na hakuna mwanachama atakayepunjika kutokana na utaratibu huo.
Mamlaka imepanga kutembelea wafanyakazi wa sekta ya madini katika juma la
kwanza la mwezi Agosti 2012 ili kutoa ufafanuzi zaidi kwa wanachama wote.

Tunatanguliza shukrani za dhati kwa ushirikiano.

Wenu.
Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii

Irene Isaka
MKURUGENZI MKUU
    kutoka mjengwablog.com

No comments:

Post a Comment