Enzi za uhai wake akiwa studio kurekodi moja ya Nyimbo zake |
Picha hii, ina utofauti. Ni kuonesha alivyokuwa akiwa binti katika Picha ndogo na sehemu kubwa akiwa Mzee |
Katika Picha hii ni wakati huo,enzi za ujana wake. |
Bi.Kidude |
BI. KIDUDE FATMA binti Baraka 'Bi kidude' ni miongoni mwa wasanii wakongwe hapa nchini wenye historia ya kipekee. Licha ya kuwa na historia ya kipekee, msanii huyo mkongwe amejipatia umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi kupitia kazi yake ya sanaa.
Bikidude anaminika kwamba ndie msanii mkongwe kuliko msanii mwingine yoyote wa kike hapa nchini.
Msanii
huyo ni muimbaji mwenye historia ya kipekee hapa nchini na kutokana na
umahiri wake wa uimbaji na amefanikiwa kutembea nchi mbalimbali za
Afrika, Ulaya na Asia kwa ajili ya kufanya kazi zake za muziki na
kuitangaza taifa kwenye jumuia za kimataifa.
Katika
siku za hivi karibuni, mkongwe huyo alikuwa akisumbuliwa na maradhi
lakini kwa sasa hali yake inaendelea vizuri ingawa hajaanza kufanya
shughuli zake za muziki.
Katika
makala haya nitazungumzia historia fupi ya msanii huyo ambaye mwishoni
mwa mwaka jana, serikali ilimtunukia nishani ya heshima kutokana na
mchango wake mkubwa kwa taifa. Nishani hiyo alitunukiwa na Rais Jakaya
Kikwete, Ikulu mjini Dar es Salaam.
Rais
Kikwete alimtunuku Bikidude na wasanii wengine nishani ya sanaa na
michezo ambayo hutolewa kwa wasanii na wanamichezo mashuhuri, ambao kazi
zao za sanaa au michezo zimeipatia sifa kubwa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
Historia
inaonyesha kwamba Bikidude ni mwimbaji wa muziki wa taarabu toka
visiwani Zanzibar. Anaangaliwa kama malkia wa muziki wa taarab na unyago
hapa nchini ambaye kipaji chake kiligunduliwa na kuimarishwa na mkongwe
wa muziki wa aina hiyo Siti binti Saad kati ya miaka ya 1880 mpaka
1950.
Bikidude alizaliwa katika kijiji cha Mfagimaringo, akiwa ni mtoto wa mfanyabiashara wa nazi enzi za ukoloni nchini Zanzibar.
Mpaka sasa
haijafahamika tarehe ya kuzaliwa ya bibi huyo kwasababu sehemu kubwa ya
historia zinazo husu historia ya maisha yake hazioani na hivyo kuwepo
na taarifa ambazo ni za kubuni.
Mwaka
2005, Bikidude alipewa tuzo ya heshima ya dunia WOMEX tuzo ambazo
zilibuniwa mwaka 1999 na mbazo wanazawadiwa watu ambao wamepata
mafanikio makubwa katika muziki au wametoa mchango mkubwa katika muziki,
umuhimu wa mtu katika jamii na hata , mafanikio ya kibiashara na kwa
upande wake ilitokana na mchango wake katika muziki na utamaduni wa
Zanzibar.
Akiwa
mdogo, Bikidude alisifiwa sana kutokana na sauti yake na katika miaka ya
1920 alianza kuimba na vikundi mbalimbali vya kiutamaduni.
Alipokuwa na umri wa miaka 13, baada ya kulazimishwa kuolewa aliamua kutoroaka na kuelekea Tanzania Bara.
Bikidude
ni moja ya waimbaji wakongwe waliozunguka nchi zote za Afrika Mashariki
akiimba taarab ambapo alitembelea miji mikubwa ya ukanda wa pwani pamoja
na bara upande wa ziwa Victoria na Tanganyika.
Mwaka 1930, alirejea Dar es Salaam na kujiunga na kikundi cha Egyptian Taarab ambacho alidumu nacho kwa miaka mingi.
Katika miaka ya 1940 alirejea Zanzibar na kujenga nyumba yake iliyokuwa ya matope na kuanza maisha mapya hapo.
Alikuwa
maarufu sana kwa shughuli za unyago ambazo ziliwaandaa masichana wadogo
kuelekea katika ubalehe na kuingia katika maisha ya utu uzima.
Ni
mtaalamu wa mambo hayo ya mila kongwe akifanya hivyo kwa wasichana
akitumia mafunzo ya kitamaduni kuwaelekeza wasichana namna ya kuishi na
waume zao na kuepuka migongano ya kifamilia na unyanyasaji wa mapenzi.
Sifa na
jina la Bikidude lilikuwa na kusifika katika jamii yote ya Zanzibari na
kuwa kielelezo cha utalii wa visiwa hivyo vya karafuu ambapo hoteli
mbalimbali kubwa na zenye hadhi ya juu visiwani humo zimekuwa zikizipa
majina migahawa ya hoteli jina la Bikidude, mfano 236 Hurumzi inatumia
jina la mgahawa wake jina la 'Kidude'.
Moja ya
nyimbo zake ambazo zilitamba na kumpatia umaarufu mkubwa mkongwe huyo ni
Muhogo wa Jang'ombe ambao ulikamata kwenye mwambao wa Afrika Mashariki.
Bikidude ni hazina kubwa na mwalimu mzuri kwani inasemekana wasanii wengi wamepata mafunzo kutoka kwake.
Pamoja na
umahiri wa msanii huyo lakini hajawahi kukumbwa na kashfa yoyote hadi
sasa hivyo amekuwa na historia ya kipekee tofauti na wasanii wa sasa.
Wasanii
wengine waliopewa nishani hiyo ni pamoja na kiongozi wa bendi ya muziki
wa dansi ya Msondo Ngoma, Muhidin Gurumo, kiongozi wa zamani wa bendi ya
Dar es Salaam International, marehemu Marijani Rajabu, aliyekuwa msanii
maarufu wa maigizo na filamu nchini, marehemu Fundi Saidi 'Mzee Kipara'
na mwanariadha mkongwe, John Steven Akwari.
Gurumo, Bi
Kidude na Akwari walihudhuria hafla hiyo ya kuvishwa nishani zao na
Rais Kikwete wakati nishani za Marijani na Mzee Kipara zilipokelewa na
watoto wao.
Bikidude
hakuweza kwenda eneo la kupokea nishani kutokana na hali ya afya yake
kutokuwa nzuri. Ilibidi Rais Kikwete amfuate mahali alipokuwa ameketi na
kumtunukia nishani yake.
Bikidude,
amedumu kwenye fani ya uimbaji kwa zaidi ya nusu karne na kwa sasa ni
msanii pekee wa taarab mwenye sifa zilizotukuka kutokana na ukongwe wake
na umahiri wake katika kuimba taarab.
Gurumo
alianza muziki 1960 na kushiriki katika bendi mbalimbali kama vile Nuta,
Juwata, Ottu, Atomic Jacc, Kiko Kids, Jamhuri Jazz, Kilwa Jazz, Rufiji
Jazz, Mlimani Park, Msondo Ngoma.
Ametunga
nyimbo nyingi zinazoelimisha jamii kuhusu kuheshimu na kufanyakazi kwa
juhudi na maarifa, kulinda uhuru wa nchi, kudumisha usawa, haki na amani
na kuwaasa wazazi kutimiza wajibu wao kwa kulea watoto na vijana
kutimiza wajibu wao.
Marehemu
Marijani, maarufu kama Jabali la Muziki, alifariki dunia mwaka 1995.
Alitoa mchango mkubwa katika tasnia ya muziki, alishiriki kutunga na
kurekodi nyimbo zaidi ya 103, ambazo zilirekodiwa RTD, nyimbo zake
zilikuwa na mafunzo mengi kwa jamii na zinaendelea kupigwa katika vituo
mbalimbali vya redio nchini.
Mzee
Kipara mwaka 1962 alijiunga na waigizaji wa Redio Tanzania, pia
ameshiriki maigizo na tamthilia nyingi za kwenye televisheni kama vile
Hujafa hujaumbifa, Fukuto, Radi, Gharika, Tufani na Tetemo.
Mzee
Akwari aliweka historia ya pekee nchini mwaka 1968 pale aliposhiriki
mbio za marathoni za Olimpiki na kuumia goti na kutoka malengelenge,
lakini aliushangaza ulimwengu alipoendelea na kumaliza mbio hizo.
Alipoulizwa, alisema 'mimi sikutumwa kuja kuanza mbio, nimetumwa
kumaliza mbio'. Maneno hayo yamekuwa yakitumika kama mifano duniani
No comments:
Post a Comment