Picha kwa hisani ya :- www.bukobawadau.blogspot.com
Baadhi ya bidhaa zinazotengenezwa na walemavu
Bango linalohamasisha kununua bidhaa zinazotengenezwa na walemavu kama hamasa ya kuwachangia kiuchumi.- Picha zote ni kwa hisani ya http://bukobawadau.blogspot.com
Aidha ;-
Katika
kusistiza kauli yake kwa vitendo juu wa walemavu katika mkoa wa Kagera
kujitegemea na kujishughulisha pia kufanya kazi mbalimbali za kujipatia
kipato na kuacha kuombaomba mitaani Mkuu wa Mkoa wa Kagera ametembelea kikundi
cha Walemavu (BUDAP) Nyamkazi katika mji wa Bukoba ili kujionea jinsi kikundi
hicho kinavyojishughulisha.
Kikundi
cha BUDAP ni kikundi cha walemavu ambao wanaendesha shughuli zao za kutengeneza
bidhaa mbalimbali za mikono na kujipatia kipato kwa kuuza bidhaa hizo hasa kwa
wageni mbalimbali wanaofika hapa mkoani katika sekta ya utalii. Bidhaa hizo ni
ngoma za asili, vidani mbalimbali pamoja na bidhaa nyinginezo mbalimbali za
mikono.
Baada
ya Mhe. Massawe kufika katika kituo hicho na kujionea jinsi kikundi hicho
kinavyojishughulisha na kazi za mikono amehaidi kuwatafutia mtaalam wa
kutengeneza andiko la mradi ili afike katika kituo hicho na kuwatengenezea
andiko ambalo atalitumia kuwatafutia wafadhili ili waweze kupata mikopo kupitia
andiko hilo.
Pia
amewasistiza walemavu hao kubuni miradi zaidi itakayowavutia wafadhili katika
kuwasaidia. Vile vile Mhe. Massawe amewahaidi kuwa ataongea na Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba ili naye awatembelee na kuona shughuli zao na
jinsi ya kuwakwamua katika kupata mtaji wa kujishulisha zaidi.
Changamoto
kubwa walionayo walemavu hao ni wenzao kuwakimbia na kutopenda kujishughulisha
na kuishia mijini na kuendelea kuombaomba ambapo wanasema kuwa walianza kikundi
na watu 20 lakini mpaka sasa wamebakia wanawake wawili na wanaume watano tu.
Mkuu
wa Mkoa wa Mkoa wa Kagera alitoa kauli ya walemavua kuacha kuwa wategezi wa
kuombaomba barabarani na mijini na kutafuta miradi ya kujishulisha ili
wajipatie kipato cha kujiinua wao wenyewe na familia zao waka, kauli hiyo
aliitoa wiki jana Alhamisi tarehe 22/11/2012 wakati akikabidhi msaada wa
baiskeli mbili kwa walemavu.
Na;
Sylvester Raphael
Afisa Habari Mkoa
KAGERA @2012
Mapema mwezi huu wa Novemba, ngarakwetublogspot ilitembelea Muleba na kuzungumza na baadhi ya walemavu ambao,tunaamini katika msaada huo unaotolewa watahusishwa.
Mlemavu Bw Kainula ambaye ni fundi wa Kushona Viatu Mjini Muleba |
Bw Twaib Abdallah Rwabasora ambaye ni fundi wa kushona Viatu,kutengeneza Simu na radio katika Kijiji cha Kasharara Muleba |
No comments:
Post a Comment