May 4, 2013

SIRIDHISHWI NA MAJIBU YA MIPAKA YA HIFADHI-DK.MBASSA MB-BIHARAMULO MAGHARIBI



Haya ndio yaliyojili wakati Mbunge wa Biharamulo Magharibi Dk.Anthony G.Mbassa akichangi Hotuba ya maliasili na utalii wiki iliyopita
·        Migogoro ya mipaka ya vijiji na maeneo ya hifadhi au maeneo tengefu.
*    Katika suala hili ameanza kwa kukataa hoja ya kamati ya bunge ya maliasili na utalii ambayo imesema kuwa yawezekana migogoro hiyo inasababishwa na wananchi kutojua maipaka ya maeneo yao na pia badhi ya wanasiasa kutumia nafasi hiyo kukuza migogoro. Ametofautiana na hoja hiyo kwa misingi mipaka hiyo lazima wakaazi waitambue tangu mapema, leo hii wananchi wa kata ya kaniha, kijiji cha kaniha na mpago wameishi pale kwa zaidi ya miaka ya 70. Mpaka wamezaliwa pale watu maarufu kama vile professa Kulikoyera Kahigi Kanalwanda mbunge wa Bukombe, amekulia hapo mpaka ameenda masomoni na sasa taifa linaona mchango wake bado utasema wananchi hawa wananishi kwenye maeneo ya hifadhi? Serikali imesajili vijiji na kaniha imesajiliwa kwa namba KGR/KIJ/694  na mpago imesajiliwa kwa namba KGR/KIJ/695. Kama serikali ipo makini ilifanyaje usajili wa vijiji hivi ili hali vipo kwenye eneo la hifadhi? Au kuna serikali mbili moja inashughulikia hifadhi na moja inashughulikia usajili wa vijiji kiasi kwamba zile document serikali moja haikujua serikali nyingine imesajili nini?      Mbaya zaidi serikali ya mkoa imepiga marufuku wananchi kulima na wameharibiwa mazao yao, ng’ombe wao wameibiwa na kutaifishwa na hawa wanasomesha watoto, wanategemea mazo kujikimu ki-uchumi sasa kwa mtindo huu wataishije? Serikali imetangaza kuwa idadi ya watu ni milioni 44.5 na kila wakifanya upimaji wa viwanja wanafanya mijini ongezeko la watu hawa vijijini haliangaliwi je wao vijijini watajitanua kwa kuelekea wapi? Wafugaji wafugie wapi? Nikamwambia waziri wakati anahitimisha aje na jibu kwa wananchi hawa ambao wameambiwa wasilime na wanaishi ndani ya hifadhi.
*    Dk. Mbasa akaongeza kuwa kuna s/m Mpago ambayo watoto mwaka huu wanahitimu darasa la saba. Na shule hiyo imesajiliwa na serikali je serikali kujenga shule pale ndani haikujua kuwa lile ni eneo la hifadhi? Kama ilijenga eneo la hifadhi serikali ilitegemea nini? Watoto wa binadamu wakasome au swala na pundamilia ndio wakasome hapo ndani ya hayo madarasa? Akamwambia waziri kuwa anahitaji i kupata jibu ni lini wizara ya maliasili na utalii watakaa na wizara ya ardhi nyumba na makazi kuja kutatua mgogoro huu walioutengeneza wao.

·        Suala la pili aliongelea kuhusu hotuba ya waziri wa maliasili na utalii kuwa zitafanyika doria 100000 (laki moja) katika maeneo ya hifadhi na mapori ya akiba.
*    Katika kuchangia hili alisema hakika hizi si doria za kuchunga au kuhifadhi wanyama wetu, bali ni doria kwa ajili ya kufukuza ng’ombe walioko jirani na mipaka ya vijiji na kuwaingiza hifadhini na hatimaya ekuwatoza pesa wananchi pasipo sababu yoyote. Akamwambia waziri akumbuke alivyofanya ziara jimboni kwake(Biharamulo), taarifa aliyompa wakiwa ofisini kwa DC(Mkuu wa wilaya) na mambo waliyomwambia akiwa kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha Ruziba, wananchi walieleza kinagaubaga kuhusu matatizo yanayo wasibu na mipaka yao na game reserves. Wanavyonyanyaswa na askari wa wanyamapori, wakikamatwa japo kwa kusingiziwa wanavyopigwa, akaomba serikali itoe kauli kwa nini hawa wanafanya kazi kinyume na sheria, utaratibu na kanuni za kazi zao? Wao wanapaswa kulinda wanyamapori na mipaka yao na si kazi ya kuchunga mifugo ya watu ndani ya hifadhi au kukamata ng’ombe kana kwamba wao ni waajiliwa wa wizara mifugo na uvuvi.

·        Kuhusu suala la fidia kwa wale wanaoharibiwa mashamba yao na wanyama au kuuawa na wanyama wakali.
*    Hapa Mh. Mbunge alihoji wizara kutotoa nyaraka kuhusu fidia wanayopawsa kulipwa waale ambao wameharibiwa mashamba yao au kuuawa na wanyama hawa. Mambo haya hayapo wazi, lakini mtu akimdhuru ngedere inakuwa hoja wakati nyani akimdhuru binadamu linakuwa jambo la kawaida. Hivyo akaomba wizara husika kutoa nyaraka hizo ikiwezekana na wabunge wapewe ilikutetea wananchi wao.

OPERESHENI YA WAFUGAJI HARAMU KAGERA.
“Mnamo mwezi novemba 2012 mkoa wa Kagera uliendesha operation ya kuondoa Wafugaji haramu ndani ya hifadhi ya hifadhi ya Burigi
a)     Je, ni wagugaji haramu wangapi walibainika katika operarion hiyo?
b)    Je, serikali imewapa fidia gani wale walioharibiwa mashamba yao na mifugo hususan kata ya Lusahunga na Kaniha?”
WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII
Mheshimiwa spika,
Kabla ya kujibu swali la MHESHIMIWA DKT ANTONY GERVASE MBASSA(MB) BIHARAMULO MAGJHARIBI naomba kutoa maelezo yafuatayo:
Ni kweli Wizara yangu mwezi Novemba, 2012 ilifanya doria maalumu kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na usalama ya mkoa wa Kagera (Jeshi la polisi,magerza, uhamiaji, TAKUKURU na JWTZ) ili kuwaondoa wafugaji haramu ndani ya mkoa wa Kagera hususan Wilaya ya Biharamulo, Muleba, karagwe na Ngara. Operation hii ilipewa jina la OMAKA- Okoa Mazingira Kagera. Umuhimu wa operarion hii ulitokana na ukweli kwamba, kulikuwepo na uingizaji wa mifugo (hasa ng’ombe), upasuaji mbao, uchomaji wa mkaa,shughuli za kilimo na uchimbaji wa madini isivyo halali ndani ya Hifadhi ya Misitu ya Mapori ya Akiba ya wanyamapori.
Mheshimiwa spika,
Baada ya maelezo hayo sasa naomba kujibu swali la MHESHIMIWA DKT ANTONY GERVASE MBASSA(MB) BIHARAMULO MAGHARIBI lenye sehemu (a) na(b) kama ifuatavyo;
a)     Katika Operesheni hiyo, wafugaji wane walikamatwa ndani ya Mapori ya Akiba ya Burigi, Biharamulo na Kimisi wakiwa na jumla ya ng’ombe 466.
b)    Kwa mujibu wa Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori na 5 ya mwaka 2009 na kanuni ya Kifuta jasho na kifuta machozi ya mwaka 2011, Serikali haitoi kifuta jasho kwa wafugaji haramu na wavamizi wanaolima ndani ya maeneo ya hifadhi.
“HAYO NDIO MAJIBU YA WIZARA KULINGANA NA SWALI UNAVYOLIONA HAPO JUU. FIKIRIA MAZINGIRA KAMA HAYO NA BAHATI NZURI ULIFIKA KWENYE MAENEO HUSIKA NA UKAONA HALI HALISI YA MAZAO YALIVYO HARIBIWA, NYUMBA ZILIVYOCHOMWA MOTO.”…. Dk Mbassa
Pamoja na majibu ya swali, Dk Mbassa alianza kuumuliza N/W kama majibu huwa wanayasoma kabla ya kwenda kuyasoma bungeni!
Alimuuliza N/W “kweli operesheni amabayo imegarimu kiasi cha zaidi ya 400 milioni Tshs halafu unakamata waafugaji 4, je zoezi hilo lilizingatia thamani ya pesa na tija iliyopatikana katika zoezi hilo?”
Mwisho akauliza wizara inatoa kauli gani kwa waliokamatiwa mifugo kwa maana ya kuifukuzia ndani ya hifadhi ili wawatoze pesa wananchi! Swali ambalo halikuwa na Jibu.
Hata hivyo,Mbunge huyo, ameahidi hivi karibuni akimaliza Vikao vya Bunge kufika jimboni kuzungumza na wananchi kuwapelekea majibu aliyopewa.
            Kila la kheri Dk.Anthony Gervase Mbassa MB Biharamulo Magharibi. Nasi tunakutakia Mafanikio katika uwakilishi wa wananchi.

No comments:

Post a Comment