March 1, 2018

Vladimir Putin asema Urusi ina kombora lisiloweza kuzuiwa

Vladimir Putin asema Urusi ina kombora lisiloweza kuzuiwa

Urusi imeunda kombora jipya ambalo haliwezi kutunguliwa na linaweza kufika pahala popote duniani, kwa mujibu wa Rais Vladimir Putin.

Bw Putin amekuwa akieleza sera zake muhimu za muhula wa nne, taifa hilo linapokaribia kufanya uchaguzi katika siku 17.
Rais huyo anatarajiwa kushinda.
Amesema kombora "halipai juu sana, ni vigumu sana kulitambua likipita, lina uwezo wa kubeba kichwa cha nyuklia na linaweza kufika popote pale. Aidha, njia linayofuata haiwezi kutabirika na adui, linaweza kukwepa vizuizi na kimsingi haliwezi kuzuiwa na mifumo ya sasa ya kinga dhidi ya makombora na hata mifumo inayotarajiwa kuundwa siku zijazo."
Katika nusu ya kwanza ya hotuba hiyo yake kwa taifa, ameahidi kupunguza viwango vya umaskini nchini humo.
Kisha, ameonesha mkusanyiko wa silaha mpya, likiwemo kombora alilosema linaweza "kufika pahala popote duniani".
Hotuba hiyo ya Bw Putin imeendelea kwa saa mbili.
Uchaguzi utafanyika mnamo 18 Machi.
   chanzo:BBCSWAHILI

www.ngarakwetu.blogspot.com

No comments:

Post a Comment