April 16, 2018

NESCH MINTEC Yatoa Semina kwa wachimbaji wa Dhahabu



Wito umetolewa kwa wachimbaji na wafanya biashara ya madini aina ya dhahabu kujenga tabia ya kutumia maabara za kisasa kupima madini hayo kabla ya kuyauza ili kuepuka upoteaji

Mkurugenzi wa Kampuni ya NESCH MINTEC TANZANIA LIMITED ambao ni wataalam wa madini aina zote katika mkutano wao na wadau wa madini kanda ya Ziwa uliofanyika  jijini Mwanza,akieleza jambo.
Wadau wa madini wakiuliza maswali



Mkurugenzi wa Kampuni ya NESCH MINTEC TANZANIA LIMITED Bwana Happines Nesvinga akitoa maelezo katika Maabara ya Kisasa,iliyopo jijini Mwanza.     


Wito umetolewa kwa wachimbaji na wafanya biashara ya madini aina ya dhahabu kujenga tabia ya kutumia maabara za kisasa kupima madini hayo kabla ya kuyauza ili kuepuka upoteaji 

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Kampuni ya NESCH MINTEC TANZANIA LIMITED ambao ni wataalam wa madini aina zote katika mkutano wao na wadau wa madini kanda ya Ziwa uliofanyika  jijini Mwanza
Mkurugenzi wa NESCH MINTEC Bw.Happines Nesvinga amesema kuwa wachimbaji wa madini wamekuwa wakiendesha shughuli zao kienyeji hali inayowakosesha mapato na kupeleka kufanya kazi kwa hasara
Insert:- Bw Happines Nesvinga

Nao baadhi ya wachimbaji walioshiriki katika mkutano huo akiwemo Mzee Cosmas Nkayamba mchimbaji wa dhahabu katika kata ya Nyakahula wilayani Biharamulo ammekiri kuwa uchimbaji wa kienyeji unawapa hasara na kuiomba serikali kuwapatia elimu ili kuboresha shughuli zao.       


www.ngarakwetu.blogspot.com

No comments:

Post a Comment