October 17, 2014

Bil 18/- kutumika kwa chanjo



BIHARMULO
Idara ya fya wilayani Biharamulop Mkoani Kagera inatarajia kutoa chanjo ya Surua na Lubera kwa wakazi wa wilaya hiyo wanaokadiriwa kuwa laki 1 na elfu 90 sawa na nusu ya wananchi wilayani humo ambao wanakadiriwa kufikia laki 3 na elfu 20

Hayo yameelezwa na mganga mkuu wa wilaya hiyo Dk. Tumpale Akim wakati akizungumza na Radio Kwizera kuhusu chanjo hiyo inayotarajiwa kuanza kesho

Dk. Tumpale ameeleza kuwa walengwa ni watoto kuanzia miezi 6 hadi miaka 14,ambapo Chanjo hiyo itawaepusha na ulemavu vifo na matatizo ya mimba kwa akina mama

Ameyaainisha maeneo itakapotolewa chanjo hiyo kuwa ni pamoja na zahanati,vituo vya afya,Hospitali,shuleni na baadhi ya makanisa yaliyoainishwa na kuridhiwa na baadhi ya viongozi wake

Aidha,mganga mkuu huyo amewataka wananchi kujitokeza kuwapeleka watoto wao katika chanjo kwaajili ya kuepuka madhara yatokanayo na ukosefu wa chanjo hiyo.  

...........................................................................................................................................
  Serikali inatarajia kutumia kiasi cha shilingi bilioni 18 kwa ajili ya chanjo ya surua na ribela inayotarajiwa kutolewa Oktoba 18 mwaka huu nchini kote.
Hayo yalisemwa na Ofisa mafunzo na mawasiliano wa idara ya kinga na chanjo wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Ibrahim Maduhu wakati wa mkutano wa kamati ya huduma ya afya ya msingi wa jiji la Tanga.
Alisema kuwa uwekezaji huo ni mkubwa kufanywa na serikali kwa wananchi wake kwa lengo la kuwapatia afya bora.
Dk Maduhu alisema, kuwa ni jukumu la kamati za afya nchini nzima
kuhakikisha wanaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa chanjo hiyo.
“Ni vema mkahakikisha watu wanajitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi hilo kwani limelenga kwa watoto kuanzia umri wa miezi tisa hadi miaka 15,” alisema
Naye mganga mkuu wa jiji hilo, Dk Asha Mahita alisema, kuwa asilimia 15 ya watoto waliopatiwa chanjo ya surua katika jiji hilo hawajajenga kinga kamili.
Alisema kuwa kampeni hiyo itawahusisha hata watoto waliopatiwa chanjo ya surua awali.
Alisema jiji hilo litakuwa na vituo 600 kwa ajili ya kutoa chanjo hiyo kwa wananchi wote

No comments:

Post a Comment