November 5, 2014

TUJIKUMBUSHE:-Mpambano wa masumbwi kati ya Mohamed Ali na George Foreman

Magazeti ya Ujerumani wiki yameandika taarifa kuhusu ushindi wa Mohammed Ali dhidi ya George Foreman
Source:http://www.dw.de/mpambano-wa-ali-na-foreman-wakumbukwa/a-18031908
Wiki hii imetimia miaka 40 tangu mabondia mashuhuri Mohammed Ali na George Foreman walipopambana katika uwanja wa kitaifa mjini Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Rumble in the jungle. Ni mpambano ulioingia katika vitabu vya historia na Mohammed Ali aliwashangaza wengi kwa kuibuka na ushindi dhidi ya Foreman ambaye mpaka wakati huo alikuwa hajawahi kushindwa ulingoni. Gazeti la "Süddeutsche Zeitung" linakumbusha namna ambavyo dunia nzima ilijaa na shauku kabla ya mpambano huo.
Mpambano huu ulikuwa mchanganyiko wa maonesho na propaganda. Dikteta Mobutu Sesse Seko alikuwa miongoni mwa wale waliowezesha tukio hilo kufanyika nchini mwake. Kwa namna hiyo alijipatia umaarufu dunia nzima. Lilikuwa moja ya matukio yaliyofuatiliwa na watu wengi zaidi katika televisheni. Hapa Ujerumani, ilibidi watu waamke saa tisa usikui ili wasipitwe.
Makala hiyo inaendelea kuelezea namna ambavyo ushindi wa Mohammed Ali uliwahimiza maelfu kuwa mabondia. Mmojawao ni Biko Botowamungu kutoka jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Alipata uraia wa Austria na mwaka 1988 kushiriki katika michezo ya olimpiki. Safari yake ya kuwa mwanandondi ilianza siku alipushuhudia mpambano kati ya Foreman na Ali kwa macho akiwa kijana wa miaka 17.

No comments:

Post a Comment