November 4, 2014

WATEMBEA KWA MGUU BARABARANI,TEMBELEENI KULIA

Mkuu wa kitengo cha usalama Barabarani,Mkaguzi wa Magari na Mtahini wa MaderevaJehi la Polis wilaya ya Biharamulo Gilbert Rutayuga

washiriki wa mafunzo 1

washiriki wa mafunzo 2
WATEMBEA KWA MGUU BARABARANI,TEMBELEENI KULIA

Na, juventus Juvenary-BIHARAMULO

Jeshi la polis kitengo cha usalama Barabarani wilayani Biharamulo Mkoani Kagera kutembelea upoande wa kulia barabarani, pamoja na kuvuka barabara katika maeneo maalum yaliyotengwa ili kuepuka ajali

Rai hiyo imetolewa na Mkaguzi wa magari na mtahini wa madereva wa jeshi hilo Bw.Gilbert Rutayiga wakati akitoa mafunzo kwa wasaidizi wa kesheria  wilayani humo

Bw. Rutayuga amesema watenbea kwamguu wawapo upande wa kulia Barabarani ni rahisi kuona na kubaini mwendo wa gari au chombo chochote kinachopita barabarani

Aidha amewataka watembea kwa mguu wanapovuka kuhakikisha wanazingatia sheria kwakugeuka kushoto na kulia kuhakikisha usalama wao pamoja na kuepuka kuvuka barabara kwa haraka wala kutembea mwendo wa pole sana.       

na wakati huo huo



Watembea kwamguu katika barabara,wametakiwa kuepuka matumizi ya vyombo vya muziki masikioni(Headphones) wanapokuwa barabarani ili kuepuka ajali na kuwa makini

Hayo yameelezwa na Mkuu wa kitengo cha Usalama Barabarani katika jeshi la Polis wilayani Biharamulo Bw.Gilbert Rutayuga wakati akitoa mafunzo kwa wasaidizi wa kisheria kutoka kata za Biharamulo

Amesema kama ilivyo marufuku kwa waendesha vyombo vya moto kutosikiliza muziki wakiwa safarini au kupiga na kupokea simu,vivyo hivyo tahadhari hiyo inatakiwa kuchukuliwa na watembea kwa mguu

Aidha,amesema ni sheria kwa watembea kwa mguu kuzingatia alama za ]barabarani,licha kuwa kuna udhaifu wa sheria kwakuwa hakuna mafunzo yanayotolewa kwa watembea kwamguu tofauti na madereva.    


No comments:

Post a Comment