February 19, 2015

TASAF KUNUSURU KAYA MASIKINI-BUHORORO NGARA

Zaidi ya kaya  masikini zipatazo 100  katika Kijiji cha Buhororo wilayani Ngara mkoani Kagera zinatarajia Kuanza kupata Ruzuku kutoka Mfuko wa hifadhi ya jamii TASAF awamu ya tatu ikiwa na lengo la kunusuru kaya masikini

Hali hiyo inatokana na hatua za awali za kutamb ua na kubaini kaya hizo katika zoezi lililofanyika hivi karibuni kijijini humo na kubarikiwa na Vikao vya halmashauri ya kijiji pamoja na mkutano mkuu wa wananchi

Mmoja wa maafisa kutoka TASAF Dk. Richard Ngowi amesema ruzuku zitatolewa kulingana na mahitaji ya kaya husika na kwamba zimegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Ruzuku muhimu na ruzuku ya masharti


Katika vikao vya awali ,afisa mwingine wa TASAF Bi. Hellen Mkongwa amewataka walengwa kuhakikisha ruzuku zitakazotolewa zinatumika ipasavyo ili kufikia malengo.
Dkt. Richard Ngowi akitamburisha Mradi katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika viwanja vya Zahanati ya Buhororo


Baadhi ya Vijana wakifuatilia Mkutano

Mmoja wa wananchi akiuliza Swali

Akina mama wakisikiliza kwa makini maelezo juu ya Mradi


Mkutano ukiendelea. Kutoka kulia ni afisa mtendaji wa Kijiji cha Buhororo Bw. Joseph Buhoma,Mwenyekiti wa kijiji Stanford Simon na Maafisa wa TASAF Hellen Mkongwa na Dk. Richard Ngowi wakitoa maelekezo kwa mmoja wa wadodosaji

   

No comments:

Post a Comment