June 8, 2016

WANANCHI WALALAMIKIA MATUMIZI YA NGUVU YA POLIS KUTAWANYA MAAANDAMANO.

WANANCHI WALALAMIKIA MATUMIZI YA NGUVU YA POLIS KUTAWANYA MAAANDAMANO.

Gari la Jeshi la Polis likipita mtaani kuwatangazia wananchi kuhusu zuio la Mkutano.


Gari la maji yanayowasha
Baadhi ya wananchi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga wamelalamikia matumizi ya nguvu za jeshi la Polis mkoani humo zilizotumika kuwatawanya wafuasi wa Chama Cha demokrasia na maendeleo CHADEMA waliokuwa katika mkutano wakidai kuwa matumizi ya nguvu yamewaathiri wananchi wasio na hatia

Wananchi hao wameeleza hayo kufuatia kitendo Jeshi hilo kutumia Mambomu ya Mchozi na maji ya kuwasha kuwatawanya watu waliokuwa katika Mkutano uliokuwa umepangwa kufanyika June 7 mwaka huu katika Uwanja wa CDT Mjini Kahama

Baadhi ya wananchi hao Alfred Festo,Yona Masabile na Augenia Masabo wamesema kuwa kitendo cha jeshi hilo kutumia nguvu kubwa kwa wananchi ni ukiukwaji wa haki za Binadamu na Vurugu kwakuwa wananchi waliokuwa katika Mkutano hawakuwa na fujo wala silaha


Hayo yameelezwa ikiwa ni siku moja baada ya Jeshi la Polis wilayani Kahama kwakushirikiana na askari wa jeshi hilo kutoka Mkoani kulipua mabomu ya kutoa machozi,kuwamwagia wananchi maji ya kuwasha na kuwasulubu baadhi ya wananchi waliokuwa Mkutanoni.

www.ngarakwetu.blogspot.com

No comments:

Post a Comment