[9:54:11 AM] Fidelis Camilius Kachinde: MISENYI
Baadhi ya wananchi wa eneo la mtukula wengi wao wakiwa
kinamama wajasiriamali na vijana wamefanya vurugu katika eneo hilo la mpakani wakipinga kitendo cha
kufungwa pingu mwenekiti wao, na kupitishwa kwa kila kibanda ili alipe fedha
alizo watoza wananchi hao wakati akiwagawia meeneo ya mda ya kufanyia biashara.
Habari kutoka huko zinasema kuwa mwenyekiti huyo aliletwa na
gari na serekali ya halmashauri ya wilaya hiyo kwa wananchi wake, ili kila mmoja
ataje kile alicho kitoa kwa mwenyekiti, naye awarudishi hapo kwa hapo.
Hata hivyo hali ilibadilika baada ya wananchi kutaka
mwenyekiti wao, waliomwita mpenda maendeleo aachiwe huru kwakufunguliwa pingu
ndipo watakapo kubali kuongelea swaala
la kilicho tolewa na kupokelwa na mwenyekiti huyo, ambapo pia ilishindikana
kuachiliwa na kurudishwa tena katika ofisi za halmashauri.
No comments:
Post a Comment