Basi lililosafirisha watu kutoka Singida-Bukoba kumsindikiza askofu Desderius Rwoma |
Gari lililokuwa katika Msfara |
Kutoka Kushoto ni Mhasham Baba askofu Severin Niwemugizi akizungumza na Askofu Rwoma mbele ya kanisa Katoliki la Biharamulo,Baada ya Misa ya asubuhi kabla ya safari kuelekea Bukoba |
Askofu Severin Niwemugizi akiwa na Askofu Rwoma-Biharamulo |
Hapa ni Kanisa kuu la Bukoba |
Maaskofu,katika Kanisa la Bukoba |
Misa takatifu ya Kumsimika Askofu Rwoma kuliongoza Jimbo la Bukoba |
April 6&7, 2013 imekuwa
zimekuwa siku za Kumbukumbu na kihistoria katika Mkoa wa Kagera hasa kwa
wafuasi wa dini ya Kikristo wa dhehebu la Katoliki. Historia hiyo ni kutokana
na Ibaada ya Kumsimika Askofu wa jimbo Katoliki la Bukoba Mhashamu Desderius
Rwoma.
Shughuli hiyo imewakutanisha
Viongozi mbali mbali wa kidini, wakiwemo Balozi wa Papa nchini Tanzania Askofu
mkuu Francisco Pardira , maaskofu wakuu,maaskofu,Mapadre,watawa na walei,lakini
pia viongozi wa serikali,Mashirika na Vyama vya siasa. Na chini kwa chini unaye msikia ni Mhashamu
Baba askofu Severin Niwemugizi wa Jimbo katoliki la Rulenge Ngara ambaye ni
makam Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania akitamburisha wageni wa sherehe hizo
Katika maadhimisho ya misa
Takatifu yaliyofanyika katika Kanisa Kuu la Jimbo la Bukoba,Viongozi wa Dini na
wa serikali walipata fursa ya kutoa ujumbe kwa waumini na wananchi
waliohudhuria katika sherehe hizo
Wa kwanza kuzungumza na umati
mkubwa wa watu waliohudhuria alikuwa askofu mstaafu wa jimbo hilo Nestory Timanywa,ambaye kwa
kiasu kikubwa alitumia muda wake kuwashukuru waumini kwa ushirikiano mkubwa
wakati wa uongozi wake
Balozi wa Papa hapa Nchini,Askofu
mkuu Francisco Pardira amewataka waumini kumuombea Askofu Rwoma ili aweze
kuitenda kazi ya bwana kwa mafanikio
Aidha, katika sherehe hizo, Rais mstaafu wa
awamu ya tatu hapa nchini Benjamin
William Mkapa alipewa nafasi ya kuzungumza na akamtaja askofu Desderius Rwoma
ambaye amehamia Bukoba akitoka Jimbo Katoliki la Singida kuwa amekuwa msaada
mkubwa uliomuwezesha kuliongoza kwa mafanikio
Taifa kwa miaka kumi
Askofu Rwoma, licha ya kuhamia
Bukoba ataendelea kuwa msimamizi wa kitume jhimbo la Singida ambalo ameliongoza
kwa miaka 14 hivi sasa
Askofu huyo alizaliwa May 08 1947
katika kijiji cha Ilogero Parokia ya Rutabo. Nikiripoti kutoka Bukoba
No comments:
Post a Comment