July 18, 2014

WANAWAKE JITOKEZENI KUGOMBEA UONGOZI SERIKALI ZA MITAA

Wito huo umetolewa kwa pamoja na Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Magharibi Dk. Athony Gervase Mbassa na Bi.Conchester Lwamulaza Mbunge wa viti maalum mkoa wa Kagera ambaye pia ni katibu wa CHADEMA mkoa na Mwenyekiti wa Baraza la wanawake BWACHA katika ziara ya Mh.Mbassa jimboni Biharamulo kuzindua na kukagua miradi ya Vikundi vya wanawake wa CHADEMA 
Mh.Conchester Lwamulaza akizungumza na Wanawake Wilayani Biharamulo
Na Juventus Juvenary-BIHARAMULO
Mwenyekiti wa Baraza la wananwake Chama cha Demokrasia na Maendeleo BAWACHA na Mbunge wa viti maalum mkoani  Kagera Bi.Conchester Lwamulaza amewataka wanawake mkoani humo kuhakikisha kuwa wanajiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura na kuytumia haki yao kikatiba kugombea nafasi mbali mbali za uongozi katika serikali za mitaa
Bi.Lwamulaza ametoa wito huo July 14, mwaka huu wakati akizungumza na vikundi vya wanawake katika ziara ya Mbunge wa jimbo la Biharamulo Magharibi Dk.Anthony Mbassa ya kutembelea vikundi hivyo
Mbunge  huyo  amesema sasa ni wakati wa wanawake kutumia fursa hiyo ya uchaguzi wa serikali za mitaa kujitokeza kugombea nyadhifa mbalimbali za kuongoza katika ngazi ya vijiji na vitongoji
Aidha,Bi. Lwamulaza amesema mbali na kujiandikisha katika daftari la wapiga kura,wanawake hao pia wanatakiwa kutunza shahada zao ili kuepuka kudanganywa na wajanja kwakununua kadi zao ili kuwakwamisha kushiriki katika uchaguzi. 
Kutoka kushoto pichani ni Bi.Devotha Stanford Mwenyekiti BAWACHA jimbo la Kyerwa,Mh.Conchester,Bi.Pendo Luis Ngonyani mwenyekiti BAWACHA Biharamulo,aliyesimama ni Dereva wa Mh.Mbunge wa Biharamulo Bw.Zephrine Stephano. Na kulia aliekaa ni Dk.Anthony G.Mbassa Mbunge katika moja ya vikao vya Vikundi vya wanawake CHADEMA GUMA
          Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Magharibi Dk.Anthony Mbassa amewataka wananchi jimboni humo kutumia  ufugaji wa nyuki kama chanzo rahisi cha mapato na njia mbadala ya utunzaji wa mazingira

Dk.Mbassa amesema hayo wakati wa ziara yake ya kutembelea na kukagua miradi inayoendeshwa na vikundi vya wanawake ndani ya jimbo hilo

Akizungumza na wanawake wa kata za Nyabusozi,Runazi na kabindi katika Vikundi vya Nyabusozi,Kiluhula,Mubaga,Nyamazike na

Kabindi,Mbunge huyo amesema ufugaji wa nyuki ni shughuli ambayo haihitaji usimamizi wa hali yajuu lakini yenye tija kubwa
Aidha,amesema ufugaji wa nyuki ni rafiki wa mazingira kwakuwa wafugaji wanakuwa makini kuchunga mizitu isiungue moto ili kuepuka hasara ya kupoteza mizinga. 

Na katika utunzaji wa Mazingira!!
Baadhi ya wakazi wa kijiji cha Kabindi Wilayani Biharamulo Mkoani Kagera wameilalamikia halmashauri ya Wilaya hiyo kukusanya mapato kutokana na ushuru wa Soko bila kurekebisha miundombinu
Wananchi hao wamesema hayo wakati wakizungumza  na Mbunge wa jimbo la Biharamulo Magharibi Dk.Anthony Mbassa katika ziara ya kutembea na kukagua shughuli za maendeleo ya Vikundi vya Wanawake katika kata hiyo
Mmoja wa wananchi hao Bw. Dismas Mathew amesema  kutokana na mapato Halmashauri inayokusanya kutokana na ushuru huo hainabudi kuyatumia katika kurekebisha miundombinu sokoni hapo kwa kujenga chanja za kupangia bidhaa
Radio Kwizera Fm imeshuhudia baadhi ya bidhaa za vyakula kama  Viazi na mihogo vikipangwa chini jambo ambalo kiafya ni hatari
Kutokana na hali hiyo Mbunge wa jimbo la Biharamulo Magharibi Dk.Anthony Mbassa amemwagiza Diwani wa kata ya Kabindi Bw.Benezett Muhoza kulifikisha katika vikao vya  maendeleo ya kata ili lijadiliwe na kutafutiwa ufumbuzi.      

Mbali na uzinduzi pamoja na ukaguzi huo,wabunge hao pia walitoa zawadi mbali mbali ikiwa ni pamoja na Kikundi cha Nyakahura kukabidhiwa Baiskeli                           

No comments:

Post a Comment