July 28, 2012

Tatizo la Maji wilayani Kibondo Mkoani Kigoma latatuliwa



Jengo la mamlaka ya maji wilayani kibondo lililoko katika chanzo cha maji Mugoboka
(picha na James Jovin )


Tatizo la maji wilayani kibondo mkoani kigoma linategemea kuisha hivi karibuni baada ya halmashauri ya wilaya hiyo kutumia zaidi ya milioni 100 kupeleka umeme katika kijiji cha Mugoboka ambapo  pampu ya umeme tayari imefungwa ili kutatua tatizo la maji wilayani humo

Ameyasema hayo mkuu wa wilaya ya kibondo bw Venance Mwamoto wakati alipokuwa akihojiwa na waandishi wa habari akiwa ofisini kwake juu ya ukosefu wa maji uliodumu kwa zaidi ya wiki tatu sasa

Amesema kuwa ukosefu wa maji unatokana na malekebisho makubwa ambayo yanafanyika katika chanzo cha mto mgoboka ikiwa ni pamoja na kubadilisha mabomba yanayopitisha maji kutokana na yale ya zamani kushindwa kuhimili nguvu za mashine mpya iliyowekwa kwa ajili ya kusukuma maji

Aidha zaidi ya shilingi milioni 200 zimetumika katika kupanua na kuongeza miundo mbinu ya maji wilayani kibondo mkoani kigoma ikiwa ni pamoja na kusogeza huduma ya maji kwa wakazi wengi zaidi

Meneja wa maji wilayani kibondo bw Matwiga Tandale amesema kuwa tayari mpango huo umeanza kufanyiwa kazi ambapo tayari
umewekwa katika bajeti ya mwaka huu inayoendelea kufanyiwa kazi jijini dare s salaam

Amesema kuwa katika kuboresha huduma ya maji visima vyenye pampu ya mkono vitabadilishwa na kuweka pampu ya umeme ili kurahisisha upatikanaji wa maji pamoja na kuboresha miundo mbinu kwa ujumla


Aidha bwa Tandale amesema pia wameomba fedha shilingi million 48 kwa ajiri ya kujengea uwezo wa kununua units za umeme pindi watakapoanza kutumia chanzo cha mgoboka ambacho kitakuwa kikitumia pampu  ya umeme

Mchakato wa kufunga pampu hiyo yenye uwezo wa kusukuma maji lita milion 3 na laki 9 kwa siku bado unaendelea katika chanzo cha maji cha mgoboka ambapo itaanza kutumika mwishoni mwa mwezi mei 


Mabomba ya maji yakiwa tayari kwa ajili ya kuanza mchakato wa kubadilisha yale ya zamani ambayo hayawezi kuhimili ukubwa wa mashine mpya yenye uwezo wa kusukuma maji mara tatu ya ile iliyokuwepo  (picha na James Jovin)



Kutokana na miundo mbinu hiyo ya maji kuboreshwa zaidi ya wakazi elfu 10,000 wilayani kibondo mkoani kigoma wanatarajia kupata huduma ya maji baada ya idara hiyo kuagiza pampu ya maji yenye uwezo wa kusukuma  lita milion 3 na laki 9 za maji kwa siku

Mhandisi wa maji wilayani kibondo bw Joseph Njela ameyasema hayo alipokuwa akiongea na radio kwizera akiwa ofisin kwake

Bw Nzela amesema kuwa  pampu ya maji iliyopo kwa hivi sasa inauwezo wa kusukuma maji lita milioni 1 na laki 3 na inauwezo wa kuhudumia watu elfu 17 hivyo baada ya kufunga pampu hiyo mpya wataongeza watumiaji  wengine zaidi ya elfu 10


Aidha amesema kuwa halmashauri imetumia zaidi ya milioni 114 kupeleka umeme katika chanzo cha maji cha Mugoboka ikiwa ni ulefu wa zaidi ya kilometa 3.2  kwa ajili ya kuanza kusukuma maji kwa kutumia umeme na kinachosubiriwa kwa hivi sasa ni pampu hiyo ambayo inategemewa kuwasili mwishoni mwa mwezi huu  


Mkuu wa wilaya ya kibondo bw Venance mwamoto akiwa anajaribu mtambo mpya wa kusukuma maji utakaoanza kufanya kazi hivi karibuni mtambo huo unauwezo wa kusukuma maji lita zaidi ya milioni 3 kwa siku (picha na James Jovin)



Katika kuboresha upatikanaji wa maji katika chanzo cha mto Mugoboka miundo mbinu imeboreshwa ikiwa ni pamoja na kuhamasisha wananchi kuacha kulima katika vyanzo vya maji ili kuboresha mazingira pamoja na kuongeza chemi chemi za maji

Mkuu wa wilaya ya kibondo bw Venance Mwamoto akiwa ameingia kwa nguvu mpya pamoja na slogani yake ya kazi kwanza maneno badae amesaidia sana katika kuhakikisha miundo mbinu hiyo ya maji inatengenezwa haraka iwezekanavyo ambapo amekuwa akifika mara nyingi katika chanzo hicho cha maji ili kuhamasisha mafundi kufanya kazi hiyo haraka iwezekanavyo.


Mkuu wa wilaya ya kibondo bw Venance Mwamoto akifuatilia hatua kwa hatua ujenzi wa miundo mbinu ya maji katika chanzo cha mto mgoboka (picha na James Jovin)

No comments:

Post a Comment