August 2, 2015

CCM NGARA-GASHAZA APITISHWA KUGOMBEA UBUNGE


Na Anord Kailembo-www.ngarakwetu.blogspot.com

Katika uchaguzi wa kura za maoni wilayani Ngara wa kumpata mgombea ubunge wa kuwakilisha chama cha mapinduzi CCM  ulikuwa kama ifuatavyo


Watangaza nia ya kugombea ubunge kupitia chama hicho ni 9 ambao ni Alex Gashaza,Elena Gozi,Issa Sama,Dr Filimon Sengati,Jerard Muhile,Sprian Muhelanyi,Radslaus Bambazi,wilidard Ntamalengero na Johakimu Nchunda.
Wanachama waliotarajiwa kushiriki katika uchaguzi huo ni 50,717
Walioshiriki uchaguzi ni 32,589
Kura zilizoharibika ni 566
Walioshiriki ni 32,028
MATOKEO NI KAMA ITUATAVYO:
MAJINA                                           KURA                   ASLIMIA
1:Alex Gashaza                              I0,814                 33.7%
2:Issa Samma                                  7,167                 22.38%
3:Ellena Gozi                                    5,474                17.09%
4:Dr.Filimon Sengati                       4,393                13.72%                 
5:Jerad Muhile                                 1,866                  5.83%
6:Spirian Muhelanyi                           927                   2.89%
7:Ladislaus Bambazi                           636                   1.99%
8:Wilbard Ntamalengelo                   390                   1.22
9:Johakimu Nchunda                          357                   1.11
Katibu wa chama hicho wilayani Ngara Bw.Jacob Makune amesema kuwa waliokuwa wakichuana kuwania nafasi ya ubunge kupitia chama hicho waungane kwa pamoja kuhakikisha wanashirikiana na Bw.Gashaza ili  mbunge wa jimbo la Ngara aweze kutokana na chama hicho.

Nao wanachama wa chama hicho walioshiriki uchaguzi huo wamesema kuwa changamoto iliojitokeza ni pamoja na kucheleweshwa kwa vifaa vya kupigia kura katika baadhi ya maeneo hali iliyopelekea wanachama wengine kushindwa kupiga kura.

No comments:

Post a Comment