October 23, 2012

Elimu ya siasa yahitajika katika ngazi za elimu

Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF wilayani Ngara Bw Ahmada abdallah


Na Shaaban Ndyamukama
Serikali imeshauriwa kurudisha elimu ya siasa katika shule za msingi na sekondari  pamoja na elimu ya watu wazima ili kizazi kipya kiweze kutambua umuhimu wa demokrasia na haki zao kisheria
Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF wilayani Ngara Bw Ahmada abdallah alitoa ushauri huo wakati akizungumza Ngara kwetu  mjini Ngara akitoa maoni yake kuhusiana na maendeleo ya jamii na demokrasia nchini hasa uhuru wa kuabudu kwa  dini ya kikristo na kiislamu 
Bw Abdallah alisema kuwa elimu ya siasa kwa shule za msingi na sekondari pamoja na elimu ya watu wazima imebaki katika takwimu  na wengi wanaoleta uvunjifu wa amani kidini na katika sheria  hawajapata elimu ya uraia kwa kujua madhara na faida za kutumia demokrasia katika kudai haki zao.
Alisema serikali pamoja na viongozi wa dini hawana budi kukaa na kujadili amani kwa waumini wao na kuweka mipaka katika kutoa maamuzi bila kutumia vurugu  na kuharibu mali za wasiohusika na tukio
Alisema kwa kuwa serikali ya Tanzania haina dini na inaongoza  watu wake wenye imani tofauti  katika dini zao ihakikishe inaweka mkazo wa sheria ili kulinda amani ya nchi inayotoa sifa kwa taifa letu duniani Aidha alishauri halmashauri ya wilaya ya Ngara kushirikisha wanasiasa katika kupanga na kuleta maendeleo ya  wananchi ili kuondoa changamoto zinazowakabili katika maeneo yao .“Viongozi wa Vyama vya siasa ni wawakilishi wa wananchi na bila kufuata tofauti za kisiasa wanao mchango wa mawazo kuhusu mahitaji ya wananchi yanayopaswa kuletwa na serikali kupitia halmashauri husika” Alisema Mwenyekiti huyo
Alidai kuwa kama miradi itakuwa wazi na kutolewa taarifa ya mapato na matumizi kwa fedha za wananchi na zinazotolewa na serikali (Ruzuku) haki itaonekana kupatikana na maendeleo yao.

No comments:

Post a Comment