February 26, 2013

USALAMA BARABARANI

Na. Mrisho Salum-Ngara

Wasfirishaji wa abiria kwapikipiki wakipata semina

Bodaboda


Watumiaji wa vyombo vya moto hasa wapanda pikipiki wilayani Ngara mkoani Kagera wametakiwa kutii sheria bila shuruti ili kuepusha mikwaruzano na vyombo vya dola nchini

wito huo umetolewa na afisa polisi jamii wilayani ngara Bw. Respikiusi John wakati akizungumza na wapanda pikipiki maarufu kama bodaboda katika mkutano wa wapanda pikipiki uliofanyika leo katika ukumbi wa community center mjini ngara

Amsema kuwa madereva wanatakiwa kuvaa kofia ngumu wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto ili kuepuka kujitokeza kwa madhara pindi ajali inapokuwa imetokea.


“baadhi ya madereva pikipiki wamekuwa wakikiuka taratibu kwa kutovaa kofia ngumu,kupakia abiria zaidi ya mmoja pamoja na kutokuwa na kofia ya abiria wake hali hii ni hatari sana”

Aidha afisa John amesema jesh la polisi halitokuwa na shida na dereva pindi anapokuwa ametii sharia za usalama barabarani.

Katika hatatua nyingine katika mkutano huo wapanda pikpiki hao wamechagua uongozi  Bw. Lameck Kashula amechaguliwa kuwa mwenyekiti Bw. Yasini Hassan akichaguliwa kuwa katibu wa umoja huo.

No comments:

Post a Comment