October 1, 2014

Mabondia Mayweather na Pacquaio wawindana

Source:DW ......Mpiganaji ngumi nyota kutoka Ufilipino Manny Pacquiao amepuuzia majigambo ya Floyd mayweather , akisema anamuonea huruma hasimu wake huyo Mmarekani na anamtaka kusoma biblia.

Mpiganaji ngumi nyota kutoka Ufilipino Manny Pacquiao amepuuzia majigambo ya Floyd mayweather , akisema anamuonea huruma hasimu wake huyo Mmarekani na anamtaka kusoma biblia.
Pacquiao amewahakikishia mashabiki wake pia kwamba atacheza kwa dakika chache mchezo wa mpira wa kikapu wakati msimu mpya utakapoanza mwezi ujao hata kama anajifua kwa ajili ya mchezo mjini Macau mwezi Novemba dhidi ya Mmarekani ambaye hajawahi kushindwa Chris Algieri.
Katika vituko vya hivi karibuni, Mayweather , ambaye hajawahi kushindwa katika mapambano yake 47, ameweka picha kadhaa katika mtandao wa kijamii , akimuonesha Pacquiao akiwa ameangushwa chini katika mapambano yaliyopita. Ameongeza kuwa Pac Man amechacha hana kitu mfukoni anasubiri malipo.

 

 

No comments:

Post a Comment