Ripoti kuhusu hali ya chakula
duniani kwa mwaka 2012 iliyotolewa leo na Shirika la Chakula la Umoja wa
Mataifa-FAO, imeonyesha kuwepo makadirio mapya ya hali ya ukosefu wa chakula
duniani.
Ripoti hiyo ya mwaka inayosisitiza
zaidi juu ya umuhimu wa kuongeza kiwango cha uwekezaji katika kilimo ili
kusaidia kupunguza njaa na umasikini duniani iliyozinduliwa leo mjini Roma,
imeonyesha kwamba mafanikio katika kupunguza tatizo la njaa katika kipindi cha
miaka 20 iliyopita yameongozeka kuliko ilivyokuwa ikiaminika hapo kabla. Kwa
mujibu wa ripoti hiyo, huenda malengo ya Maendeleo ya Milenia kuhusu kupunguza
njaa na umaskini yatafikiwa ifikapo mwaka 2015, kutokana na makadirio mapya ya
lishe kuboreshwa kwa mbinu na mikakati mbalimbali. Mafanikio mengi yalipatikana
hasa katika kipindi cha mwaka 2007 na 2008 na tangu wakati huo, mafanikio ya
kupunguza njaa yalianza kupungua. Hata hivyo, idadi ya watu wanaokabiliwa na
tatizo kubwa la ukosefu wa chakula cha kutosha bado iko juu na jitihada za
kumaliza tatizo la njaa bado linabakia kuwa changamoto kubwa duniani.
Watu 870 wanakabiliwa na njaa
duniani
Mkurugenzi Mkuu wa FAO, José Graziano da Silva |
Akizungumzia ripoti hiyo, Mkurugenzi
wa idara ya Kilimo, Maendeleo na Uchumi katika Shirika la Chakula la Umoja wa
Mataifa, Kostas Stamoulis amesema kuwa kiasi watu milioni 870 duniani
wanakabiliwa na njaa na kati ya hao, milioni 852 ni kutoka mataifa
yanayoendelea. Stamoulis amesema idadi hiyo ni sawa na asilimia 12.5 ya watu
duniani kote wanaokabiliwa na njaa. Ripoti ya mwaka huu pia inaelezea mchango
wa ukuaji wa uchumi katika kupunguza tatizo la ukosefu wa chakula cha kutosha.
Ukuaji endelevu wa kilimo mara nyingi umekuwa na ufanisi kwa watu maskini kwa
sababu wengi wao wanaishi katika maeneo ya vijijini na wanategemea kilimo kama
sehemu kubwa ya maisha yao. Hata hivyo, ukuaji huo haumaniishi kwamba ni lazima
uongeze lishe bora kwa watu wote. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, sera na mipango
ambayo itahakikisha ukuaji wa lishe bora, ni pamoja na kusaidia kuongeza malazi
tofauti, kuimarisha upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama, usafi wa
mazingira na huduma nzuri za afya pamoja na kuwaelimisha watumiaji kuhusu lishe
bora ya kutosha na suala la kutoa malezi bora kwa watoto.
Ukuaji wa uchumi unachukua muda
kuwafikia maskini
Njia ya kukausha mahhindi |
Aidha, ripoti hiyo ya Shirika la
Chakula la Umoja wa Mataifa kwa mwaka 2012 inafafanua kwamba ukuaji wa uchumi
unachukua muda kuwafikia watu maskini na kwamba huenda usiwafikie kabisa wale
walio maskini zaidi duniani. Kutokana na hali hiyo, ulinzi wa kijamii ni muhimu
katika kutokomeza tatizo la njaa haraka iwezekanavyo. Ripoti hiyo imebaini kuwa
maendeleo ya haraka katika kupunguza tatizo la njaa na utapiamlo yanahitaji
serikali kuchukua hatua na kuweka mikakati ili kuhakikisha zinatoa huduma nzuri
za kijamii ndani ya mfumo wa utawala kwa kuzingatia uwazi, ushirikishwaji,
uwajibikaji, utawala wa sheria pamoja na haki za binaadamu.
Source:DW
Mwandishi: Grace Patricia Kabogo/FAO
Website,RTRE
Mhariri:Yusuf Saumu
Mhariri:Yusuf Saumu
No comments:
Post a Comment