March 12, 2013

POLISI WAUA MAJAMBAZI 7 BIHARAMULO



 Hadi jana mchana,
Miili ya watu 7 wanaosadikiwa kuwa majambazi waliouawa kwa kupigwa risasi na askari wa jeshi la Polisi wilayani  Biharamulo Mkoa wa kagera iilikuwa iukiendelea kuhifadhiwa  katika Hospitali teule ya wilaya hiyo baada ya ndugugu zao kukosekana

Kabla ya kifo chao, Watu hao 7 wakiwa na silaha za Kivita wameuawa kwa kupigwa risasi na askari wa jeshi la Polisi wakati wakiwa katika msitu wa kijiji cha Mavota wakati wakijitayarisha kuvamia na kufanya uharifu katika Mgodi wa dhahabu TULAWAKA wilayani Biharamulo Mkoani Kagera  march 10 mwaka huu

Akizungumza na Ngara kwetu Mganga Mkuu wa Hospitali teule ya wilaya hiyo Dk. Gresmus Sebuyoya alisema Hospitali yake inaendelea kuhifadhi miili hiyo kwakuwa ndugu wa marehemu hawajafika kuitambua miili ya ndugu zao
Hata hivyo, Dk sebuyoya alisema Hospitali hiyo inafanya mawasiliano na Kamanda wa jeshi la Polisi Mkoa wa kagera Phillip Kallangi ili kupata Kibali cha kufanya mazishi ya miili hiyo,kuepusha kuharibika vibaya na kutoa harufu kwakuwa iliharibiwa vibaya kwa risasi

Tukio la majambazi hao kuuawa limetokea March 10 mwaka huu na kuthibitishwa na  Kamanda wa Jeshi la Polis Mkoani Kagera Phillip Kalangi
Aidha Kamanda Kalangi amesema kufanikisha udhibiti wa uharifu na kuuawa kwa majambazi hao,kumetokana na taarifa ziliripotiwa na wananchi kwa jeshi la Polis.

1 comment:

  1. Nafurahia kupata hii blog!Nilikuwa najaribu kuangalia kama kuna kitu kama hii blog,basi leo nimefurahi kuiona.Asante kwa kutujulisha habari za huko sie tulioko nje ya Ngara.Kila jema na endelea kutujuza mambo ya huko hasa mikakati ya maendeleo mfano,mikutano ya vijiji,Kata,Tarafa,Wilaya na jinsi wanavyopanga maendeleo.

    ReplyDelete