December 28, 2013

CHADEMA YASEMA USHINDI 2013 NI LAZIMA,YAWAHIMIZA WANANCHI KUJITOKEZA KATIKA UCHAGUZI

Meza kuu, Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa baraza la vijana BAVICHA wilaya Nestory Mashishanga,katikati ni mwenyekiti CHADEMA Wilaya Stanford Kennedy Festo,anaye fuata ni Mjumbe wa kamati John Simon Malanilo na kulia ni Mke wa Malanilo Bi. Juliana Mbowe

Dk. Ssebuyoya akiwa na wajumbe wa kamati ya CHADEMA wilaya, wakifuatilia mkutano

Mwenyekiti wa tawi la Mukabenga akifungua mkutano



Kutoka kushoto ni Bi.Elda Brighton,Katikati ni Dk. Gresmus Ssebuyoya na kulia ni Bi.Magdalena Ntazimila katika mkutano wa hadhara -Mwivuza


NGARA
Wajumbe wa kamati kuu ya chama cha demokrasia na maendeleo Chadema wilayani Ngara wamewataka wananchi wilayani humo wenye sifa za kuchagua na kuchaguliwa kuwa viongozi kutumia kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu ujao

Wajumbe hao Dr. Gresmus Ssebuyoya na John simon Malanilo wametoa wito huo kwa nyakati tofauti katika mikutano ya hadhara iliyofanyika katika Vijiji vya Mwivuza na kirushya

Akizungumza katika mkutano uliofanyika katika kitongoji cha Mukabenga,mmoja wa wajumbe hao Bw. John Simon Malanilo amesema ni haki kwa kila mwananchi kuchagua na kuchaguliwa

Kwa upande wake Dk. Gresmus Ssebuyoya amesema kupitia chaguzi hizo,CHADEMA itapata viongozi makini watakaoharakisha maendeleo ya jimbo la Ngara,hivyo ni fursa kwa wananchi kushiriki kikamilifu.    

No comments:

Post a Comment