December 27, 2013

MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA NGARA(CCM)2010 AHAMIA CHADEMA

Dk Peter Bujari. Picha kutoka Maktaba

DK Bujari wakati wa kampeni kuelekea uchaguzi mkuu 2010. Picha kutoka Maktaba
MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA NGARA(CCM)2010 AHAMIA CHADEMA
Na, Juventus Juvenary
ALIYEKUWA mgombea ubunge jimbo la Ngara kupitia Chama cha Mapinduzi CCM katika uchaguzi mkuu uliopita 2010 Dk. Peter Bujari ametangaza rasmi kukihama chama chake na kujiunga na chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA
Akizungumza na wandishi wa habari nyumbani kwake katika kijiji cha Bikiriro wilayani Ngara,Dk Bujari alisema ameamua kujiunga na CHADEMA baada ya kuridhishwa na sera na uwajibikaji ndani ya chama hicho
Alisema kuwa atakabidhi kadi ya CCM kwa Mwenyekiti wa CHADEMA taifa Bw. Freeman Mbowe ambaye anatarajiwa kuwa wilayani Ngara Jumamosi Disemba 28 mwaka huu
Awali taarifa kutoka kwa mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA Bw. Stanford Kennedy Festo zililidokeza gazeti hili kuwa Dk. Bujari alikuwa na mpango wa kuhamia Chadema na kwamba suala hilo lingetangazwa rasmi baadae
Hata hivyo alisema kuondoka kwake CCM na kwenda CHADEMA ni kutaka kuleta mabadiliko katika upinzani dhidi ya Chama cha Mapinduzi, na kwamba atahakikisha kuwa wafuasi aliokuwa nao wanahamia kwenye chama hicho

Dk Bujari alisema Chama cha Mapinduzi CCM kina muda mrefu tangu kuanzishwa kwake lakini kimeshindwa kuwajibika na kuwaletea maendeleo wananchi hali ambayo yeye kama mzalendo hawezi kuivumilia.

No comments:

Post a Comment