November 13, 2012

Saba wafa maji wilayani Muleba




Na: Shaaban Ndyamukama
WATU saba wanaokadiriwa kuwa na umri wa miaka  kati ya 30 na 40 wamefariki dunia huku wawili wakinusurika baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama katika kisiwa cha Hifadhi ya Taifa Rubondo  ndani ya ziwa viktoria wilaya ya Muleba mkoani Kagera
Akiongea kwa njia ya simu Jumanne wiki hii  diwani wa kata ya Ikuza wilayani Muleba Fortunatus Martha Wazia alisema kuwa watu hao waliondoka katika kisiwa cha ikuza kwenda kwenye hifadhi ya Rubondo Novemba nane na walipita njia za panya wakiwepa walinzi wa hifadhi wasije kukamatwa na wamepatikana wakiwa maiti Novemba 10 ya jumamosi wiki iliyopita

Wazia amewataja waliofariki dunia kuwa ni  Baruya Masala mkazi wa Muganza wilayani Chato ,Alex Mwita mkazi wa Tarime ,Kipara Kasukari  wa kata ya mushabago wilayani Muleba na mwingine amejulikana kwa jina moja la Niko mkazi wa sengerema
Wengine  ni Obedia Yohana mkazi wa Muganza wilaya ya Chato,Juma Kengere mkazi wa Itale  wilayani Chato na wa saba ametambuliwa kwa jina moja la Robart mwenyeji wa wilayani Biharamulo.Amesema kuwa katika kuopoa maiti ndani ya maji jumatatu wiki hii waliotambuliwa na jamaa zao wamesafirishwa kwa kuzikwa walikotokea na maiti tatu ndizo zimezikwa katika kisiwa cha Ikuza wilayani Muleba
Alisema wavuvi hao walikwenda kuvua samaki wakiwa ni wavuvi haramu katika hifadhi ya Rubondo  na boti yao haikuwa imara ilianza kuvuja wakati wakirejea kisiwani Ikuza na hatimaye kuzama ndani ya ziwa hilo  nyakati za usiku na wawili kati ya tisa waliokuwa ndani ya boti ndio walioogelea hadi nchi kavu mwaloni na kutoa taarifa.

"Siku ya tukio kwa maelezo ya walionusurika ambao hakuwataja majina yao inasemekana hapakuwa na hali mbaya ya hali ya hewa ispokuwa boti yao haikuwa imara na iliingiwa na maji wakashindwa kutoa maji hayo na kwa wingi wao na mizigo walianza kuzamana kufariki dunia."Alisema Wazia

Aidha Diwani huyo amewashauri wavuvi katika ziwa Victoria kufanya kazi zao kwa kutumia njia harali na vyombo vyao kukaguliwa na malaka husika ili kuepusha madhara  katika vyombo vyao na maisha yao  ikiwa ni pamoja na kuimalika kwa ulinzi katika shughuli zao
Kamanda wa jeshi la  polisi mkoani Kagera  Bw Philipo Karangi amethibitisha kutokea kwa vifo vya watu hao na kwamba jeshi la polisi linaendelea kufanya upelelezi kuhusiana na mazingira yaliyopelekea kutokea kwa tukio hilo.
www.ngarakwetublogspot.com

No comments:

Post a Comment