Kardinali Jorge Bergoglio wa Argentina
amechaguliwa kuongoza Kanisa Katoliki Duniani, akiwa ni wa kwanza kutoka
barani Amerika na wa kwanza kutoka nje ya Ulaya kwa zaidi ya miaka
1,000.
Baada ya kuchaguliwa na makardinali wenzake 115, Kardinali Jorge Bergoglio (76) alichagua kufahamika kwa jina la Francis I.
Maelfu ya mahujaji, watalii na waumini wa Kanisa
Katoliki waliokuwa wamejazana katika Viwanja vya Kanisa la Mtakatifu
Petro, Vatican kushuhudia moshi mweupe uliofuka saa 4:00 usiku kwa saa
za Afrika Mashariki kuashiria kuchaguliwa kwake, waliripuka kwa shangwe,
nderemo na vifijo.
Muda mfupi baada ya moshi huo kutoka, kardinali
mmoja alisimama katika ‘varanda’ ya Kanisa la Mtakatifu Petro na
kutangaza “Habemus Papum” (tumepata papa mpya).
Papa Francis I alikuwa miongoni mwa waliokuwa wanawania nafasi hiyo na papa anayeondoka, Benedict XVI mwaka 2005, ambapo aliripotiwa kuibuka wa pili.
Papa Francis I alikuwa miongoni mwa waliokuwa wanawania nafasi hiyo na papa anayeondoka, Benedict XVI mwaka 2005, ambapo aliripotiwa kuibuka wa pili.
Kabla ya kuchaguliwa kwake, Papa Francis I ambaye
kwa wadhifa wake pia anakwenda kuwa Askofu wa Roma, alikuwa Askofu Mkuu
wa Jimbo la Buenos Aires, Argentine na kwa muda wote wa utumishi wa
utumishi alikuwa huko huko nyumbani.
Anakuwa Papa wa 266 kuwahi kuongoza kanisa hilo lenye waumini zaidi ya bilioni 1.2 duniani.
Baada ya kutangazwa kwake, Papa Francis I alijitokeza kuzungumza kwa mara ya kwanza kama Askofu wa Roma.
Baada ya kutangazwa kwake, Papa Francis I alijitokeza kuzungumza kwa mara ya kwanza kama Askofu wa Roma.
Akiwa amechaguliwa katika awamu ya tano ya upigaji
kura, inaelezwa kuwa alikuwa miongoni mwa mapapa waliochaguliwa kwa
haraka baada ya muda mrefu, akiwa sawa na Benedict XVI (2005) na Pius
XII aliyechaguliwa mwaka 1939.
Mshindi alitakiwa kupata kuta 77 au robo tatu ya makardinali 115 walioshiriki uchaguzi huo.
Papa Francis I anachukua nafasi iliyoachwa na Papa Benedict XVI aliyejiuzulu Februari 28, mwaka huu, ikiwa ni miaka 600 tangu Papa wa mwisho kujiuzulu.
Papa Francis I anachukua nafasi iliyoachwa na Papa Benedict XVI aliyejiuzulu Februari 28, mwaka huu, ikiwa ni miaka 600 tangu Papa wa mwisho kujiuzulu.
Yeye ni nani
Papa Francis I, ni Papa wa kwanza kutoka Shirika la Jesuit ambaye ametumia muda wake mwingi wa utumishi nyumbani Argentina.
Papa Francis I, ni Papa wa kwanza kutoka Shirika la Jesuit ambaye ametumia muda wake mwingi wa utumishi nyumbani Argentina.
Anafahamika kwa utumishi uliotukuka kwa uangalizi
wa kanisa na mapadri, mambo ambayo yanatajwa kuwa sifa kubwa ya
kuchaguliwa kuwa Papa.
Papa huyo amedumu katika maisha ya kufundisha na
kuongoza mapadri. Amefanya kazi Amerika ya Kusini ambako kuna Wakatoliki
wengi. Kardinali Bergoglio anatambulika kwa kutamadunisha Kanisa la
Argentina, lililokuwa miongoni mwa makanisa ya kihafidhina huko Amerika
Kusini.
Amechagua jina la Papa Francis I, chini ya uangalizi wa Mtakatifu Francis wa Assisi.Alizaliwa Buenos Aires katika familia ya mfanyakazi wa reli. Alipata upadrisho mwaka 1969.
Aprili 15, 2005, mwanasheria wa haki za binadamu alimfungulia mashtaka ya jinai kwa kushirikiana na maofisa wa jeshi kuwateka mapadri wawili wa Jesuit mwaka 1976, akiwa kiongozi wao aliwafukuza katika utumishi kutokana na migogoro katika jumuiya hiyo
No comments:
Post a Comment