December 6, 2013

MAJAMBAZI WAMVAMIA MFANYA BIASHARA NA KUONDOKA NA FEDHA,WAMJERUHI KWA MAPANGA MWINGINE



Na,Juventus Juvenary-Ngara

Kundi la watu wanaosadikiwa kuwa majambazi limemvamia mfanyabiashara katika kijiji cha Rulenge wilayani Ngara mkoani Kagera na kumpora fedha kiasi cha shilingi laki nane
Tukio hilo limetokea Alhamisi Disemba 5 mwaka huu majira ya saa 4 usiku,ambapo baada ya kutimiza azima yao walikimbilia kusikojulikana
Afisa mtendaji wa kijiji cha Rulenge Bw Edson Metusela Gachocha amemtaja mfanyabiashara aliyevamiwa kuwa ni Ibrahimu Abdalah Bijampora , nakuongeza kuwa majambazi hayo  yalivamia nyumba ya Bw. Bijampora yakiwa na Silaha za moto na jadi ambapo yalivamia  sebuleni wakati yeye na familia yake wakifuatilia Taarifa ya habari kwenye Luninga
“Mara baada ya kuingia walianza kushambuliana naye ambapo aliwataka wamuachie awatafutie fedha na walipokubali aliingia ndani na kufanikiwa kuwatoroka , ndipo walimkaba mke wake na kuondoka na fedha hizo”alisema
Hata hivyo mmoja wa wafanya biashara wa mji mdogo wa Rulenge Ruguge Nzutu Ruguge amewataka wajasiriamali kuimarisha ulinzi wa maeneo ya shughuli zao ili kuhakikisha usalama unapatikana katika sikukuu za chrismas na mwaka mpya
Katika miaka ya hivi karibuni imekuwa kawaida ya kipindi chwa mwishoni mwa mwaka kuelekea siku za Krismas na mwaka mpya matukio ya uharifu hasa uporaji wa fedha kwa wafanya biashara kutokea, hali inayolitaka jeshi la Polisi pia kuimarisha usalama

Katika hatua nyingine Mwanamke mmoja aliyetambulika kwa jina la Revina Alex (36) mkazi wa kijiji cha Rulenge wilayani humo  amelazwa katika Hospitali ya Misheni Rulenge baada ya  kujeruhiwa na majambazi kwa kumkata mapanga kichwani 
Diwani wa kata ya Rulenge Bw Hamis Baliyanga amesema kuwa mwanamke huyo alijeruhiwa na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi waliovamia nyumbani kwake  na kupora mali ambayo thamani yake haijajulikana
Baliyanga amesema kuwa majambazi hayo yalimvamia saa nane usiku kupitia mlango wa nyuma ya nyumba ambapo walifungua mlango kwa kutumia nondo na kuingia ndani
Jeshi la polisi wilayani Ngara limethibitisha kutokea kwa matukio yote mawili  na kwamba linaendelea na msako mkali kuwabaini wahusika pamoja na kutoa wito kwa wananchi kujenga tabia ya kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa za viashiria vya uharifu

No comments:

Post a Comment