July 5, 2014

KERO YA MAJI NYAKANAZI-BIHARAMULO

Haya ndio maisha ya wakazi wa Nyakanazi. wana pata tabu sana kuhusu Maji Safi na Salama.
 Pichani ni mtoto mdogo kama anavyoonekana akishikilia Baiskeli wakati akimsubiri mama yake ambaye wakati napiga picha hii alikuwa akimtwisha nddo ya maji mwenzake,
Chanzo cha maji kikiwa kimefunikwa
 Hii ni staili ya utunzaji wa vyanzo vya maji. Wananchi wamebuni njia hii . licha ya kuwa maji si safi na Salama lakini huu ni mkakati madhubuti wa kutunza vyanzo ili kuepusha wanyama kuingia majini na kuchafua zaidi
 Kijana mdogo akichota maji  na kuyajaza kwenye plastiki la lita 20
 Pamoja na matumizi ya maji haya, ni sehemu pia ya watoto wanapochezea kama wanavyoonekana pichani

 Ujenzi wa kuhifadhi chanzo hiki unaendelea. Ni hatari sana kwa watoto wadogo kuchezea maeneo hayo. kama picha inavyoonekana akiteleza kidogo lazima adodoke,ni hatari
Mwanablogu mwenzangu Bahat Anastars,ambaye ni Driver wa shirika lisilo la kiserikali CHEMA wilayani Biharamulo ambaye ndiye aliyewezesha usafiri kufika eneo hilo. Pichani anaonekana akitoa msaada kumtwisha ndoo ya maji mmoja wa mabinti waliofika kuchota maji.
NENO:- Mmoja wa wananchi waliozungumza nami katika eneo hili na kukataa jina lake nisiliandike amesema:-NI AIBU KWA TAIFA KAMA TANZANIA LENYE RASILIMALI NYINGI,UTAJIRI WA HALI YA JUU WATUWAKE KUNYWA MAJI KAMA HAYA .

No comments:

Post a Comment